MWIGIZAJI zao la mchezo wa Bongo Dar es Salaam, Flora
Mvungi amevishwa pete ya uchumba na Hamis Baba ‘H-Baba’ baada ya kuishi kinyumba
na mwanaume huyo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
Akiongea na mwandishi wa habari hii, Flora alisema safari yao ya kuelekea kuoana na H-Baba ilipigwa vita na wengi lakini kwa sasa anamshukuru Mungu dalili za ndoa zinanukia.
“Kuna baadhi ya ndugu waliweka pingamizi mimi na H-Baba kufikia hatua hii, nilisubiri sana, hatimaye jamaa kaleta posa nyumbani na kanivisha pete ya uchumba,” alisema Flora.
0 comments:
Post a Comment